Mikopo hutolewa kwa mwanachama na wafanyakazi wa Lulu Saccos. Mkopaji atajaza fomu ya mikopo na atatoa mchanganuo wa mkopo, mfan...
Read MoreLulu Saccos Ltd ni chama cha ushirika wa akiba na mikopo kinachofanya shughuli zake katika mkoa wa Mbeya, chama hiki ni muungano wa wafanya bihashara na wajasiliamali wanaofanya shughuli zao katika mkoa wa Mbeya. Aidha, LULU SACCOS LTD ilianzishwa kwa wazo lililotokana na kikundi cha kijamii chenye wanachama 50, wenye asili ya Tarafa mbili za Lupila na Lupalilo zilizopo wilayani Makete katika Mkoa wa Njombe waishio Mbeya Mjini. Wanachama hao waliungana kwa lengo la kusaidiana katika masuala ya kijamii.
LULU SACCOS LTD ilisajiliwa na Mrajis Msaidizi wa vyama ushirika mkoa wa Mbeya tarehe 13/03/2007 na kupatiwa namba ya usajili MBR 737. LULU SACCOS ilianza na mtaji wa shilingi milioni kumi na tatu kwa mgawanyo ufuatao: Hisa 750 zenye thamani ya Tsh 7,500,000/= Akiba za wanachama Tsh 3,500,000/= Viingilio Tsh 2,000,000/=
Lulu Saccos tupo Soweto Mbeya Mjini, tunatazamana na barabara kuu ya Tanzania Zambia